Magazeti leo Julai 29,2025

TUME Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC) imesema kwa mara ya kwanza wafungwa na mahabusu watapiga kura kwenye Uchaguzi Mkuu wa mwaka huu.
Mkurugenzi wa Uchaguzi INEC, Ramadhani Kailima alisema hao Dodoma wakati akiwasilisha mada ya maandilizi ya uchaguzi na ushiriki wa vyama vya siasa kwenye mkutano wa kitaifa wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC).






Kailima alisema katika uchaguzi wa mwaka huu wafungwa na mahabusu watapiga kura ya urais pekee na maeneo hayo hakutakuwa na mawakala wa vyama vya siasa kutokana na usalama.

Aidha, alisema vyama vya siasa vinapaswa kuwasilisha tume majina ya wagombea wabunge na madiwani kabla au ifikapo Septemba 28, mwaka huu “Kwa upande wa majina ya wabunge na madiwani wa viti maalumu, yanatakiwa kupelekwa mwezi mmoja kabla ya uchaguzi mkuu,” alisema Kailima.

Alisema itakapotokea wagombea watakapojitoa na kubakia mmoja siku moja hadi tatu kabla ya uchaguzi INEC inaweza kupeleka mbele uchaguzi ili kuipa nafasi kuandaa upya karatasi za kupiga kura.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news