Naibu Katibu Mkuu Omolo atembelea banda la BoT maonesho ya Sabasaba

DAR-Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha, Bi. Jenifa Christian Omolo, ametembelea banda la Benki Kuu ya Tanzania katika Maonesho ya 49 ya Biashara ya Kimataifa (Saba Saba), yanayoendelea katika viwanja vya Mwalimu Julius Nyerere, Dar es Salaam.
Katika ziara hiyo, Bi. Omolo ameshuhudia jinsi wataalamu wa Benki Kuu ya Tanzania wanavyotoa elimu kwa wananchi kuhusu masuala mbalimbali, yakiwemo uwekezaji katika dhamana za serikali za muda mfupi na mrefu, mchakato wa ulipaji wa gawio kwa wawekezaji, pamoja na fursa za masomo zinazotolewa na Chuo cha Benki Kuu ya Tanzania.
Amesisitiza umuhimu wa elimu kwa umma kuhusu masuala ya kifedha, ili kuwawezesha wananchi kushiriki kikamilifu katika maendeleo ya uchumi wa taifa.
Maonesho hayo yanayofanyika kuanzia tarehe 28 Juni hadi 14 Julai 2025, yanabebwa na kauli mbiu “ Maonesho ya Biashara ya Kimataifa “Saba Saba” Fahari ya Tanzania.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news