Dkt.Mwinyi achangia shilingi milioni 50 katika Mfuko Maalum wa Kampeni za CCM

DAR-Makamu Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Zanzibar, Rais wa Zanzibar Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Dkt. Hussein Ali Mwinyi amechangia Shilingi Milioni 50 katika Mfuko Maalum wa Kampeni za CCM kwa ajili ya Uchaguzi Mkuu Oktoba 29, 2025.
Dkt. Mwinyi ametoa mchango huo katika Harambee hiyo iliyozinduliwa na Mwenyekiti wa CCM Taifa, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, iliyofanyika tarehe 12 Agosti 2025 katika Ukumbi wa Mlimani City, jijini Dar es Salaam.
Mwenyekiti wa CCM Taifa Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, naye amechangia Shilingi Milioni 100 katika Harambee hiyo, huku viongozi mbalimbali wa Serikali, Taasisi, Kampuni, Mashirika, makada na wanachama wa CCM wakitoa michango yao kwa moyo wa uzalendo.

Katika Harambee hiyo, jumla ya Shilingi Bilioni 56 zimekusanywa, na ahadi za michango yenye thamani ya Shilingi Bilioni 30 zimetolewa na taasisi na watu binafsi walioshiriki hafla hiyo.
Harambee ya kuchangia Mfuko Maalum wa Kampeni za CCM itaendelea hadi tarehe 27 Agosti 2025.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news