CHAMA Cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Kongwa kimetangaza kuanza tena mchakato wa kuchukua na kurejesha fomu za kuwania nafasi ya Ubunge wa Jimbo la Kongwa, kufuatia kifo cha aliyekuwa Spika wa Bunge na Mbunge wa jimbo hilo, Job Ndugai kilichotokea Agosti 6,2025.


Taarifa hiyo imeeleza kuwa, gharama za fomu zitaendelea kuwa kama zilivyoanishwa kwenye Kanuni za Uongozi katika Vyombo vya Dola toleo la 2025, huku ikisisitiza masharti kwa waombaji ikiwemo kuwa wanachama hai wa CCM wenye akili timamu na waliolipia ada.Aidha, imekataza wanachama kuandaa misafara ya magari, pikipiki, baiskeli, ngoma au matarumbeta kwa ajili ya kumsindikiza mgombea kuchukua fomu, pamoja na kuwaleta wapambe kwa lengo la kufanya sherehe.
Tags
Kurasa za Magazeti
Kurasa za Mbele na Nyuma za Magazeti
Magazeti
Magazeti ya Leo
Magazetini
Magazetini leo
Yaliyojiri Magazetini Leo























