Mkurugenzi wa Shirika la Mawasiliano Tanzania (TTCL), CPA (T) Moremi Marwa, amesema katika mwaka wa fedha 2025/2026 Serikali kupitia shirika hilo imepanga kujenga zaidi ya minara 1,400 ya mawasiliano nchini, ikianza na minara 600 mwaka huu, na mingine 850 kufuata mwaka 2026/2027.
CPA Marwa ameyasema hayo Agosti 24, 2025, katika banda la TTCL kwenye Kikao Kazi cha Wenyeviti wa Bodi na Watendaji Wakuu wa Taasisi za Umma (CEOs Forum 2025) kinachoendelea katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha AICC jijini Arusha, kilichofunguliwa rasmi na Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Philip Isdori Mpango.
Tags
Kurasa za Magazeti
Kurasa za Mbele na Nyuma za Magazeti
Magazeti
Magazeti ya Leo
Magazetini
Magazetini leo
Yaliyojiri Magazetini Leo

















