Magazeti leo Agosti 7,2025

TANZANIA imepata heshima nyingine kubwa kimataifa baada ya Bi.Irene Eliakim Maswi kuchaguliwa kuwa Mkurugenzi wa Kanda ya Afrika wa Shirikisho la Kimataifa la Vyama vya Wanafunzi Madaktari (IFMSA) kwa kipindi cha 2025/2026.
Bi.Maswi ambaye alianza safari yake ya uongozi katika Chuo Kikuu cha KCMC kwa kushika nafasi ya Rais wa Chama cha Madaktari Wanafunzi Tanzania (TAMSA), ameendelea kupeperusha vyema bendera ya Tanzania katika majukwaa ya kimataifa sekta ya afya.
Uteuzi wake umetajwa kuwa alama ya matumaini kwa wanafunzi wa tiba nchini na barani Afrika, ukionyesha wazi kuwa vijana wa Kitanzania wana uwezo wa kushika nafasi muhimu duniani na kuchangia kwa vitendo katika maendeleo ya sekta ya afya.

TAMSA na jumuiya ya wanafunzi wa tiba nchini wamepongeza mafanikio hayo wakisema yanatia moyo kwa kizazi kijacho cha wataalamu wa afya kushiriki katika uongozi na mabadiliko ya kijamii barani Afrika na duniani kote.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news