Hongereni Benki Kuu ya Tanzania kwa kuendelea kuelimisha wananchi-RC Mtaka

MBEYA-Mkuu wa Mkoa wa Njombe, Mhe. Anthony Mtaka ametembelea banda la Benki Kuu ya Tanzania (BoT) tawi la Mbeya katika Maonesho ya Wakulima ya Nanenane yanayoendelea katika Viwanja vya John Mwakangale jijini Mbeya.
Katika ziara hiyo, Mhe. Mtaka alipata maelezo kutoka kwa wataalamu wa Benki Kuu kuhusu majukumu yake mbalimbali, hususan utekelezaji wa sera ya fedha na udhibiti wa mfumuko wa bei, pamoja na hatua nyingine zinazolenga kuhakikisha uthabiti wa uchumi wa nchi.
Aidha, ameipongeza Benki Kuu kwa jitihada zake za kuelimisha umma na kuhimiza ushiriki wa wananchi katika maendeleo ya uchumi wa taifa.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news