Mwanahabari Erick David Nampesya afariki

DAR-Mwandishi mkongwe wa habari na aliyewahi kuitumikia BBC World Service nchini Tanzania, Erick David Nampesya, amefariki dunia huko Kibamba, Dar es Salaam.Awali, alikuwa akipatiwa matibabu katika Hospitali ya Mloganzila jijini humo.
Kwa mujibu wa taarifa kutoka kwa jamaa zake wa karibu, marehemu Nampesya alikuwa akisumbuliwa na ugonjwa wa Homa ya Ini (Hepatitis), ingawa pia aligundulika kuwa na vidonda vya tumbo.

Nampesya aliyezaliwa mwaka 1969, na aliyekuwa akiripotia Idhaa ya Kiswahili ya BBC, alikumbwa pia na majeraha makubwa kichwani baada ya kuanguka vibaya, anguko ambalo alilielezea mwenyewe takribani miezi miwili kabla ya kifo chake.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news