Rais Dkt.Mwinyi atoa wito kwa wanasiasa nchini

ZANZIBAR-Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Alhaj Dkt. Hussein Ali Mwinyi, amewasihi wanasiasa kutumia majukwaa ya kisiasa kutangaza sera za vyama vyao kwa wananchi badala ya kueneza siasa za chuki.
Rais Dkt. Mwinyi ameyasema hayo leo Agosti 15,2025 alipotoa salamu kwa waumini wa dini ya Kiislamu baada ya Sala ya Ijumaa na dua maalum ya kuwaombea viongozi wakuu wa nchi, iliyofanyika katika Msikiti wa Shaafi, Mbuyu Mnene, Mkoa wa Mjini Magharibi.
Amesema, ni vema wanasiasa kuhubiri amani na kueleza namna watakavyowatumikia wananchi baada ya kupata ridhaa ya kuwaongoza, badala ya kutangaza siasa za chuki, matusi na mifarakano ndani ya jamii.

Pia, Rais Dkt. Mwinyi amewasisitiza viongozi wa dini na waumini kuiombea nchi amani hasa katika kipindi hiki ambacho kimebakia miezi michache kabla ya Uchaguzi Mkuu. Amesema bila amani hakuna jambo lolote la maendeleo linaloweza kufanikishwa.
Kwa upande mwingine, Rais Dkt.Mwinyi ameeleza kuwa kila raia mwema ana wajibu wa kuhakikisha amani ya nchi inadumu wakati wote.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news