MOROGORO-Katika Maonesho ya Nanenane Kanda ya Mashariki jamii imepata elimu kuhusu mchango wa Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) katika kukabiliana na athari za mabadiliko ya tabianchi kwa wakulima wadogo.
Vilevile namna ya kutumia taarifa za utabiri wa hali ya hewa kwa kupanga shughuli za kilimo ili kuongeza tija na kupunguza hasara.
Vilevile namna ya kutumia taarifa za utabiri wa hali ya hewa kwa kupanga shughuli za kilimo ili kuongeza tija na kupunguza hasara.Elimu hiyo ilitolewa kupitia matangazo Mubashara MVIWATA FM, yakirushwa kutoka Banda la Mamlaka ya Hali ya Hewa katika Maonesho ya Nanenane yanayofanyika Uwanja wa Mwalimu Nyerere mkoani Morogoro, hatua iliyosaidia kuwafikia wakulima wengi zaidi hata nje ya uwanja wa maonesho.
Tags
Habari
Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA)
Maonesho ya Nanenane
Tanzania Meteorological Agency (TMA)

.jpg)


