Viongozi, wananchi waendelea kujifunza mengi banda la BoT maonesho ya Nanenane Zanzibar

ZANZIBAR-Viongozi mbalimbali pamoja na wananchi wameendelea kutembelea Banda la Benki Kuu ya Tanzania kwenye Maonesho ya Nane Nane Zanzibar yanayofanyika katika viwanja vya Dole-Kizimbani, visiwani Unguja, Zanzibar. Miongoni mwa viongozi hao ni pamoja na Waziri wa Maji, Nishati na Madini Zanzibar, Mhe. Shaibu Hassan Kaduara, Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Nyumba Zanzibar, Bw. Sultan Said Suleiman na Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya Zanzibar, Kanali Burhan Zubeir Nassor.

Katika maonesho hayo Benki Kuu inaelimisha umma kuhusu majukumu yake katika kusimamia ukuaji endelevu wa uchumi na ustawi wa sekta ya fedha nchini.
Maonesho hayo yenye kaulimbiu “Kilimo ni Utajiri, Tunza Amani- Tulime Kibunifu” yalianza tarehe 1 Agosti na yanatarajia kufikia tamati tarehe 14 Agosti, 2025.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news