Zanzibar inahitaji fursa za uwekezaji-Rais Dkt.Mwinyi

ZANZIBAR-Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Mheshimiwa Dkt.Hussein Ali Mwinyi amesema kuwa,Zanzibar inahitaji fursa za uwekezaji katika sekta mbalimbali ikiwemo Uchumi wa Buluu, sekta ya miundombinu, afya pamoja na fursa za kibiashara kwa ajili ya kuongeza thamani ya bidhaa za karafuu na mazao ya baharini.
Rais Dkt. Mwinyi ameyasema hayo alipokutana na Balozi wa Tanzania nchini Italia, Mhe. Mbarouk Nassor Mbarouk, aliyefika Ikulu Zanzibar leo Agosti 19,2025 kumuaga baada ya kuteuliwa hivi karibuni na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan.
Aidha, Rais Dkt. Mwinyi ameeleza kuwa sera ya diplomasia ya uchumi ndiyo iliyopewa kipaumbele hivi sasa katika Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, hivyo ni vema Balozi huyo kuifanyia kazi sera hiyo ili uchumi wa Tanzania hususan Zanzibar uendelee kuimarika.
Naye Balozi Mbarouk amemhakikishia Rais Dkt. Mwinyi kwamba ataendelea kuimarisha zaidi mahusiano pamoja na kutafuta fursa mbalimbali za ushirikiano.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news