Balozi Mwamweta amtaka mwanariadha Gabriel Geay na wenzake kuiwakilisha vyema Tanzania jijini Berlin



BERLIN-Balozi wa Tanzania nchini Ujerumani, Mhe. Hassani Mwamweta amewataka wanariadha wanaoshiriki mashindano ya BMW Berlin-Marathon mwaka 2025 kutetea heshima ya nchi kwa kuhakikisha kuwa wanafanya vizuri katika mashindano hayo, yatakayofanyika Berlin Septemba 21, 2025.
Balozi Mwamweta kauli hiyo ameitoa alipokutana na wanariadha hao, wakiongozwa na Bw. Gabriel Geay ofisini kwake jijini Berlin leo Septemba 19, 2025.
Balozi Mwamweta amesema, mashindano ya BMW Berlin-Marathon ni miongoni mwa mashindano makubwa ya riadha Duniani ambayo mwaka huu yatajumuisha washiriki 80,000 kutoka duniani kote, hivyo ushindi wa aina yotote utailetea heshima na kuitangaza nchi ya Tanzania ulimwenguni.
Balozi Mwamweta amewatakia heri wakimbiaji hao katika mashindano hayo na kuwaahidi kuwapa ushirikiano unaohitajika ili waweze kuwakilisha vyema bendera ya Taifa. #BerlinMarathon

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news