Dkt.Biteko atembelea banda la BoT katika Maonesho ya Teknolojia ya Madini Geita

GEITA-Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dkt. Doto Biteko, ametembelea banda la Benki Kuu ya Tanzania (BoT) katika Maonesho ya Teknolojia ya Madini yanayoendelea katika viwanja vya Dkt. Samia Suluhu Hassan mkoani Geita.
Mara baada ya kuwasili, Dkt. Biteko alipokelewa na Meneja wa Idara ya Mawasiliano wa Benki Kuu, Bi. Victoria Msina, ambaye alimueleza kwa kina kuhusu huduma na elimu zinazotolewa kwa wananchi wanaotembelea banda hilo.

Katika ziara hiyo, Dkt. Biteko alipata fursa ya kujionea namna wataalamu wa BoT wanavyotoa elimu kwa wananchi kuhusu majukumu ya Benki Kuu, ikiwemo kudhibiti mfumuko wa bei, kusimamia sekta ya fedha, na kulinda thamani ya shilingi ya Tanzania.
Benki Kuu imeendelea kushiriki katika maonesho mbalimbali nchini kwa lengo la kuendeleza mawasiliano na jamii, pamoja na kushirikiana na wadau mbalimbali ili kuongeza uelewa wa wananchi kuhusu sekta ya fedha na nafasi yake katika kukuza uchumi wa taifa.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news