Bodi ya Wataalam wa Ununuzi na Ugavi nchini (PSPTB) imefanya tathmini ya bajeti na kuweka mikakati mipya ya kuboresha utendaji kazi kwa mwaka wa fedha 2025/2026, lengo likiwa kuongeza ufanisi katika sekta ya ununuzi na ugavi.
Akizungumza katika kikao kazi cha Baraza la Wafanyakazi kilichofanyika mkoani Morogoro, Mkurugenzi Mtendaji wa PSPTB, Bw. Godfred Mbanyi, amesema kikao hicho kimekuwa fursa ya kupitia utekelezaji wa malengo ya mwaka uliopita na kupanga mikakati mipya ya kufanikisha malengo ya mwaka ujao.
Tags
Kurasa za Magazeti
Kurasa za Mbele na Nyuma za Magazeti
Magazeti
Magazeti ya Leo
Magazetini
Magazetini leo
Yaliyojiri Magazetini Leo














