Magazeti leo Septemba 12,2025

Mgombea Urais wa Tanzania kupitia Chama cha ACT-Wazalendo, Luhaga Mpina leo Septemba 11, 2025 ameshinda kesi ya kupinga kuzuiwa kurejesha fomu za uteuzi wa mgombea Urais aliyofunguliwa dhidi ya Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC) na mahakama kuamuru taratibu ziendelee zilipoishia.













Kesi hiyo namba 21692/2025, iliyofunguliwa na Bodi ya Wadhamini wa ACT Wazalendo pamoja na Lugaha Mpina, ikipinga uamuzi wa INEC kumuengua mgombea wao wa Urais, katika orodha ya wagombea.

Jopo la majaji watatu, Abdi Kagomba, Evaristo Longopa na John Kahyoza ndiyo waliokuwa wakisikiliza kesi hiyo. Majaji hao wamesema INEC ni Tume huru na haikupaswa kusikiliza maelekezo ya mtu au taasisi yoyote.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news