Magazeti leo Septemba 3,2025

SHIRIKA la Viwango Tanzania (TBS) limewataka wazalishaji, wasambazaji, wafanyabiashara na waingizaji wa bidhaa nchini kuhakikisha bidhaa wanazozalisha au kuuza zinakidhi matakwa ya viwango na ubora ili kulinda afya za wananchi na kutimiza azma ya Serikali ya kuhakikisha upatikanaji wa bidhaa bora sokoni.
Akizungumza Septemba 1, 2025 na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam, Meneja Ukaguzi na Utekelezaji wa Sheria wa TBS, Bi. Nuru Mwasulama amesema kuwa, bidhaa yoyote kabla ya kutumika inapaswa kukidhi matakwa ya usalama na ubora na kupata ruhusa rasmi ya kutumika.
Aidha, Bi. Nuru amebainisha kuwa,TBS imeendelea kufanya ukaguzi sokoni ili kubaini bidhaa hafifu zisizokidhi viwango na kuondoa sokoni zile ambazo hazifai kwa matumizi ya wananchi.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news