Magazeti leo Septemba 8,2025

CHAMA cha African Democratic Alliance (ADA-TADEA) kimesema, ili kuimarisha Muungano wa Tanganyika na Zanzibar ulioasisiwa mwaka 1964 watajenga daraja kutoka Bagamoyo hadi Zanzibar kurahisisha usafiri kati ya Bara na Zanzibar ili wananchi waweze kusafiri muda wowote bila vikwazo.
Ilani ya uchaguzi ya chama hicho imeeleza kuwa,daraja hilo la muungano litakuwa daraja la viwango vya hali ya juu.

Pia,imesema chama hicho kitajenga madaraja mengine Ziwa Nyasa, Victoria na Kamanga kwa ajili ya kuunganisha Wilaya ya Sengerema na Nyamagana.

Vilevile,ilani hiyo imeeleza kuwa serikali yake itayafanyia ukarabati madaraja makubwa kwenye njia kuu ya Dar es Salaam hadi Kigoma, Dar es Salaam hadi Tunduma na Mtwara hadi Mbamba Bay.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news