Msajili wa Hazina afanya mazungumzo na TRC, LATRA

DODOMA-Msajili wa Hazina, Bw. Nehemiah Mchechu amekutana na kufanya mazungumzo na Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Reli Tanzania (TRC), Mhandisi Machibya Shiwa pamoja na Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini (LATRA), Bw.Abdallah Mhagama.
Mazungumzo hayo, ambayo pia yalihusisha wataalamu kutoka taasisi hizo tatu, yalifanyika katika ofisi za LATRA jijini Dodoma, na yalilenga kuboresha utendaji kazi wa TRC.
Ofisi ya Msajili wa Hazina inasimamia jumla ya taasisi na kampuni 308 ambazo Serikali ina hisa.
Kati ya hizo, taasisi 252 – zikiwemo TRC na LATRA – ni zile ambazo Serikali inamiliki hisa nyingi, huku 56 zikiwa ni kampuni ambazo Serikali inamiliki hisa chache.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news