Simba SC yamtangaza Hemed Suleiman (morocco) kuwa kocha wa muda

DAR-Klabu ya Simba SC imethibitisha kumteua kocha wa Timu ya Taifa ya Tanzania, Hemed Suleiman (morocco) kuwa kocha wa muda 'Caretaker' wa klabu hiyo kwenye mechi za Kimataifa baada ya Kocha, Fadlu Davids kusitisha mkataba na Kocha Selemani Matola kuwa na kadi nyekundu.
Hayo ni kwa mujibu wa taarifa ya leo Septemba 22, 2025 na uongozi wa klabu hiyo,imeeleza kuwa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) limemruhusu Kocha morocco kujiunga na Wekundu hao wa Msimbazi katika kipindi hiki ambacho klabu inakamilisha taratibu na mchakato wa kocha wa kudumu.

Morocco ataliongoza benchi la ufundi kuelekea mchezo wa marudiano wa Ligi ya Mabingwa barani Afrika dhidi ya Gaborone United FC Septemba 28, 2025.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news