BoT yaendelea kuelimisha wananchi katika maonesho ya madini Geita

GEITA-Wataalamu wa Benki Kuu ya Tanzania wameendelea kutoa elimu kwa wananchi mbalimbali wanaotembelea banda la Benki Kuu ya Tanzania (BoT) kwenye Maonesho ya Teknolojia ya Madini yanayoendelea katika viwanja vya Dkt. Samia Suluhu Hassan, mkoani Geita.
Katika banda hilo, wananchi wamepata fursa ya kufahamu majukumu makuu ya Benki Kuu yakiwemo kusimamia sera ya fedha, kudhibiti mfumuko wa bei, kusimamia sekta ya benki na taasisi za kifedha pamoja na kulinda thamani ya shilingi ya Tanzania.
Aidha, wananchi wamepata elimu ya kutambua alama za usalama zilizopo kwenye noti halali za shilingi, jambo linalosaidia kupunguza hatari ya kupokea fedha bandia.

Vilevile, elimu imetolewa kuhusu mpango wa ununuzi wa dhahabu unaoratibiwa na Benki Kuu kwa lengo la kuongeza akiba ya fedha za kigeni na kuimarisha thamani ya shilingi yetu.
Maonesho haya yamekuwa fursa kwa wananchi kuelimishwa pia kuhusu mifumo ya malipo ya taifa, umuhimu wa kuweka akiba, na namna ya kuwekeza katika dhamana za serikali.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news