Dimitar Pentev ndiye Meneja na Kocha Mkuu wa Simba SC

DAR-Klabu ya Simba SC imemtambulisha rasmi Dimitar Pentev, raia wa Bulgaria, kuwa Kocha Mkuu na Meneja mpya wa klabu hiyo ya jijini Dar es Salaam.
Ujio wa Pentev unakuja kuziba nafasi iliyoachwa wazi na Fadlu Davids, ambaye alijiunga na klabu ya Raja Casablanca ya Morocco hivi karibuni.

Kabla ya kujiunga na Simba, Pentev alikuwa Kocha Mkuu wa Gaborone United ya nchini Botswana, ambako alionekana kufanya kazi nzuri na kuacha alama katika soka la ukanda huo.

Uzoefu wake katika soka la Afrika unatajwa kuwa moja ya sababu zilizomvutia Simba SC kumleta Msimbazi.

Mashabiki wa Simba na wadau wa soka kwa ujumla wanafuatilia kwa karibu kuona mwelekeo mpya chini ya Pentev, huku wengi wakitarajia atakuja kuongeza ushindani na kuleta mafanikio zaidi kwa klabu hiyo kubwa nchini.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

Know matter how large or small your business is, advertising here