Magazeti leo Oktoba 4,2025

Bodi ya Ligi Kuu Tanzania (TPLB) imemfungia mchezaji wa Klabu ya Young Africans, Ibrahim Abdullah (Bacca) kutoshiriki mechi tano kutokana na kosa la kumkanyaga kwa makusudi mchezaji wa Mbeya City, Ibrahim Ame, tukio lililofanyika katika mechi ya Ligi Kuu iliyochezwa Jumanne ya Septemba 30, 2025 na kumalizika kwa sare ya 0-0.
TPLB imeeleza kuwa, rafu hiyo ilikuwa ya hatari na ingeweza kuhatarisha usalama wa mchezaji huyo.

Sambamba na hilo, Mwamuzi wa mchezo huo, Omary Mdoe kutoka Tanga, naye amepewa adhabu ya kukaa nje kwa mizunguko mitano ya Ligi Kuu kwa kushindwa kutafsiri sheria ipasavyo katika mchezo huo, hali iliyochangia kutochukuliwa hatua stahiki dhidi ya tukio hilo uwanjani.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news