Kutoka darasani hadi Benki Kuu,wanafunzi 350 wapata uelewa mpya kuhusu majukumu ya BoT

DAR-Wanafunzi wapatao 350 kutoka Shule ya Sekondari Bagamoyo, Kisarawe II na Baobab wametembelea Benki Kuu ya Tanzania (BoT) jijini Dar es Salaam, ambapo walipata fursa ya kujifunza kwa undani kuhusu majukumu ya Benki Kuu katika kusimamia uchumi wa nchi.
Aidha, wanafunzi hao walipata mafunzo kuhusu utambuzi wa alama za usalama katika noti za Tanzania na namna bora ya kuzitunza, ili kuepuka uharibifu wa fedha hizo.
Vilevile, wanafunzi walitembelea Makumbusho ya Benki Kuu ya Tanzania, ambako walijifunza kuhusu historia ya fedha nchini, historia ya Benki Kuu pamoja na mageuzi na maendeleo mbalimbali ya sekta ya fedha yaliyotekelezwa chini ya usimamizi wa Benki Kuu tangu kuanzishwa kwake mwaka 1966.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news