Magazeti leo Oktoba 11,2025

MKUU wa Mkoa wa Arusha, CPA Amos Gabriel Makalla, amemshukuru Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuboresha miundombinu ya viwanja vya ndege vya Arusha na Manyara, hatua inayowezesha huduma za ndege kufanyika saa 24 na kurahisisha upatikanaji wa huduma kwa watalii.
Akizungumza Oktoba 10, 2025, wakati wa kilele cha Wiki ya Huduma kwa Wateja, Makalla alisema maboresho hayo yameongeza ushindani na ubora wa huduma, sambamba na kuchochea ongezeko la watalii mkoani humo. “Dk. Samia amekuwa na dhamira ya kukuza utalii kupitia miundombinu rafiki inayoruhusu ndege kubwa kutua kwa saa 24,” alisema.

Aliwataka watumishi na wadau wa sekta ya usafiri wa anga kutoa huduma bora na kwa weledi ili kukuza utalii na uchumi wa mkoa. Meneja wa Uwanja wa Ndege wa Arusha, Edga Mwankuga, alisema wiki ya huduma kwa mteja imetoa fursa kwa wateja kutoa maoni na kusaidia kuboresha huduma, akisisitiza kuwa “mteja ni moyo wa taasisi.”

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news