Magazeti leo Oktoba 15,2025

CHUO Kishiriki cha Elimu Mkwawa (MUCE), kikiwa chini ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), kimepongeza juhudi kubwa za Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa uwekezaji mkubwa katika sekta ya elimu, kupitia Mradi wa Elimu ya Juu kwa Mageuzi ya Kiuchumi (Higher Education for Economic Transformation-HEET Project).
Katika taarifa iliyotolewa Rasi wa Chuo Kishiriki cha Mkwawa, Profesa Method Semiono ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya kumbukizi ya Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere amesema kuwa mradi huo ni matokeo ya dhamira ya Serikali ya kuendeleza elimu ya juu ili kuchochea mageuzi ya kiuchumi nchini.

Alisema kuwa mradi wa wa HEET ambao serikali ya Rais Samia umekuwa na Uwekezaji wa Kimkakati katika elimu nchini ikiwa unatekelezwa kwa miaka mitano (2021/2022–2025/2026) unafadhiliwa na Benki ya Dunia na unalenga kuboresha ubora wa elimu ya juu nchini.

Profesa Semioni alisema kuwa kupitia mradi huo MUCE imetengewa kiasi cha Dola za Kimarekani milioni 8 (sawa na Shilingi Bilioni 18.6 kwa ajili ya utekelezaji wa miradi mbalimbali ya kimkakati.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news