Magazeti leo Oktoba 22,2025

Mgombea urais kupitia Chama cha NLD, Mhe. Doyo Hassan Doyo, ameendelea na kampeni zake za lala salama wilayani Masasi, katika viwanja vya Soko la Mkuti, Masasi Mjini.
Akiwahutubia mamia ya wakazi wa Masasi, Mhe. Doyo ameahidi kuwa serikali yake, endapo atapewa ridhaa na wananchi, itarejesha reli ya Masasi, Dar es Salaam, ambayo ilisitisha shughuli zake mwaka 1972.

Amesema kuwa reli hiyo ilikuwa uti wa mgongo wa uchumi wa kusini, na kufufuliwa kwake kutachochea kwa kiasi kikubwa maendeleo ya kijamii na kiuchumi. “Kupitia reli hii, wakulima wa korosho, na mazao mengine ya biashara wataweza kusafirisha bidhaa zao kwa gharama nafuu hadi masoko makubwa ndani na nje ya nchi,” amesema Mhe. Doyo.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news