Mbaroni kwa uchochezi na kuhamasisha maandamano yasiyo halali nchini

DODOMA-Jeshi la Polisi Tanzania limekanusha taarifa zinazosambazwa kupitia vyombo vya habari zikidai kuwa watu saba wamekamatwa katika mazingira ya kutatanisha, likisema kuwa waliokamatwa walitiwa nguvuni kwa mujibu wa sheria kutokana na tuhuma za uhalifu, zikiwemo za uchochezi na kuhamasisha maandamano yasiyo halali.
Kupitia taarifa yake kwa umma iliyotolewa Oktoba 17, 2025, Makao Makuu ya Polisi Dodoma, kupitia Msemaji wake DCP David Misime, jeshi hilo limesema,miongoni mwa watu sita waliotajwa katika taarifa hizo, walikamatwa kwa mujibu wa taratibu za kisheria.

Ni kutokana na ushahidi uliokuwa umekusanywa kabla ya kukamatwa kuhusiana na tuhuma mbalimbali za kihalifu.

Jeshi hilo limefafanua kuwa,watuhumiwa hao walikamatwa kwa kosa la matumizi mabaya ya mitandao kwa kufanya uchochezi na kuhamasisha maandamano kinyume cha sheria.

"Wakati wa ukamataji watu walishuhudia na baadhi ya viongozi wao walifika katika ofisi za makamanda wa polisi mikoa na vituo vya polisi kuwaulizia, na walijulishwa kuwa watu sita wanashikiliwa na walielezwa tuhuma zao," taarifa hiyo imeeleza.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

Know matter how large or small your business is, advertising here