Naibu Waziri Chumi akutana na Balozi wa Cuba nchini

DAR-Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Chumi, amekutan na kuzungumza na Balozi wa Cuba nchini, Mhe. Yordenis Despaigne Vera, katika Ofisi ndogo za Wizara jijini Dar Es Salaam.
Mazungumzo hayo yalilenga kujadili namna ya kuendelea kuimarisha ushirikiano wa kidiplomasia kati ya Tanzania na Cuba.

Katika mazungumzo hayo, Mhe. Chumi amesisitiza umuhimu wa Serikali za Tanzania na Cuba kuweka mikakati madhubuti ya kuendeleza ushirikiano wa kidiplomasia.
Ameishukuru Serikali ya Cuba kwa kuendelea kushirikiana karibu na Tanzania hasa katika sekta ya afya, elimu, viwanda na diplomasia.

“Tanzania imenufaika na madaktari wa kujitolea kutoka Cuba, fursa za masomo kwa wanafunzi katika taaluma za afya na sayansi, pamoja na uanzishaji wa kiwanda cha viuatilifu Kibaha mkoani Pwani, na msaada katika sekta ya kilimo.

"Kimsingi, mataifa haya yameimarisha ushirikiano wa kimataifa katika kutetea haki za nchi zinazoendelea na kusisitiza mshikamano wa kimataifa,"alifafanua Mhe.Chumi.

Naye Balozi wa Cuba nchini Mhe. Yordenis Vera ameishukuru Tanzania kwa kuendeleza ushirikiano na nchi yake, na emeelezea umuhimu wa kukuza ushirikiano katika diplomasia ya Uchumi husuani katika sekta za biashara, viwanda, teknolojia, utamaduni na michezo.
Tanzania na Cuba zimekuwa na uhusiano wa karibu na kindugu tangu enzi za kupigania uhuru ambapo Hayati Baba wa Taifa Mwalimu Julius Nyerere na Hayati Fidel Castro walijenga misingi ya uhusiano ya kidugu inayozingatia usawa, mshikamano na maendeleo ya pamoja.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news