Tanzania kuendelea kushirikiana na Comoro sekta ya afya

ANJOUAN-Balozi wa Tanzania nchini Comoro, Saidi Yakubu amewahahakikishia wananchi wa Comoro kuwa Tanzania itaendelea kushirikiana nao katika Sekta ya Afya ikiwa ni pamoja na mafunzo kwa wataalamu wake.
Balozi Yakubu ameyasema hayo wakati wa hafla ya kufunga Kambi Tiba iliyofanyika katika Hospitali ya Bambao ambapo ilielezwa kuwa, jumla ya wagonjwa 3,653 wamepatiwa huduma za matibabu na kati yao 20 walifanyiwa upasuaji muhimu kunusuru afya zao.
Gavana wa Kisiwa hicho,Dkt.Zaidou Youssouf akiambatana na Mshauri wa Rais wa Comoro (Siasa),Mheshimiwa Humed Msaidie aliahidi kutembelea Tanzania mwezi Januari,2026 ili kuweka sawa makubaliano ya ushirikiano ikiwa ni pamoja na utaratibu bora wa kesi za rufaa kwa wananchi wa Anjouan.

Kwa upande wake,mwakilishi wa Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya Tanzania,Dkt.Asha Mahita alieleza kuwa, fursa za ushirikiano katika mafunzo na usambazaji wa dawa na vifaa tiba ni miongoni mwa vipaumbele vya kuzingatiwa kwa sasa.
Kambi hiyo ya matibabu imetekelezwa na madaktari 52 kutoka hospitali tano za Muhimbili,Benjamin Mkapa, Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete,Taasisi ya Saratani ya Ocean Road na Taasisi ya Mifupa ya Muhimbili na pia Bohari Kuu ya Dawa Tanzania.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news