VIDEO:Derek Murusuri afichua siri kuelekea Uchaguzi Mkuu

DEREK Kaitira Murusuri ni mwandishi, mwanahabari, na mshauri wa maendeleo nchini Tanzania, anayeheshimika kwa maandiko na uchambuzi wake kuhusu ukombozi wa kiuchumi na uongozi barani Afrika.
Akiwa na uzoefu mkubwa katika masuala ya kisiasa, Derek Murusuri pia amejikita katika kazi za ushauri, utafiti na mafunzo katika nyanja mbalimbali za maendeleo na siasa ndani na nje ya Tanzania.

Mwaka huu alizindua kitabu kipya kinachochambua kwa kina falsafa ya uongozi ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan.

Kitabu chake kilichopewa jina la Samia na Falsafa ya Samiaolojia", kinachambua falsafa ya "4Rs" ya Rais Samia yaani Maridhiano, Ustahimilivu, Mageuzi, na Ujenzi Upya kama nguzo kuu za uongozi wake.

Murusuri ameendelea kushiriki kikamilifu kama mchambuzi wa masuala ya kisiasa, hususan katika kipindi cha kuelekea uchaguzi mkuu wa Tanzania.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news