ZECO kuzima umeme baadhi ya maeneo Zanzibar kesho

ZANZIBAR-Shirika la Umeme Zanzibar (ZECO) limewatangazia wateja wake kuhusu kuendelea kwa kazi ya ujenzi wa njia mpya ya umeme, ikiwa ni sehemu ya juhudi za kuboresha miundombinu na kuongeza ubora wa huduma ya umeme visiwani.
Kutokana na kazi hiyo, ZECO litalazimika kuzima umeme kwenye baadhi ya maeneo ili kuruhusu utekelezaji salama wa shughuli hiyo. Umeme utazimwa kwa njia za msongo wa kilovolti 33 na 11, hasa kwa kuwa njia mpya inapita karibu na ile ya zamani inayosambaza umeme katika ukanda wa Kaskazini Unguja.

Taarifa ya ZECO imeeleza kuwa umeme utakatwa kesho Jumapili, tarehe 5 Oktoba 2025 kuanzia saa 4:00 asubuhi hadi saa 9:00 alasiri.

Maeneo yatakayoathirika ni: Mwanyanya, Bububu, Kwa Nyanya, Chuini, Mfenesini, Kitope, Mahonda, Donge, Mkokotoni, Tumbatu, Shangani Shamba, Kivunge, Fukuchani, Kidoti, Tazari, Kigunda, Mwambale, Kendwa, Nungwi, Kizimbani, Dole, Kianga, Masingini, Mtofaani, Hawai na Kinuni.

ZECO inaomba radhi kwa usumbufu utakaojitokeza na inawaomba wateja kuwa wavumilivu wakati zoezi hilo likiendelea kwa ajili ya huduma bora zaidi.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news