DAR-Benki Kuu ya Tanzania (BoT) imefanya mauzo ya Dola za Marekani milioni 20 katika Soko la Jumla la Fedha za Kigeni (IFEM), ikiwa ni sehemu ya utekelezaji wa Sera ya Ushiriki wa Benki Kuu katika Soko la Fedha za Kigeni ya mwaka 2023.
Mauzo hayo yametekelezwa kupitia mnada wa ushindani, ambapo kiwango cha wastani cha ubadilishaji kilikuwa Shilingi 2,447.55 kwa Dola moja ya Marekani.
"Katika ushiriki huu, Benki Kuu imeuza Dola za Marekani milioni 20.00 kupitia mnada wa ushindani kwa kiwango cha wastani cha kubadilisha fedha za kigeni cha Shillingi 2,447.55 kwa Dola moja ya Marekani. Lengo la mnada huu lilikuwa ni kuongeza ukwasi katika soko la fedha za kigeni."

