Mabaki ya mwili wa Mtanzania Joshua Loitu Mollel yawasili nchini Tanzania

KILIMANJARO-Mabaki ya mwili wa Kijana Joshua Loitu Mollel aliyeuwawa nchini Israel na wapiganaji wa Hamas Oktoba 07, 2023 yamewasili leo Novemba 19, 2025 katika kiwanja cha Ndege cha kimataifa cha Kilimanjaro (KIA).
Mabaki ya mwili huo yamepokelewa na Ujumbe wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ukiongozwa na Naibu katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Said Shaib Mussa na Balozi Silima Haji Kombo.
Mabaki ya Kijana Joshua Mollel yanatarajiwa kuzikwa kesho Novemba 20, 2025 mtaa wa Njiro, katika kata Orkesumet Wilaya ya Simanjiro mkoani Manyara.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news