Magazeti leo Novemba 10,2025

Mkurugenzi wa Uendeshaji wa Lake Oil Group, Stephen Mtemi, ameeleza kusikitishwa kwake na kitendo cha watu kuchoma vituo vya mafuta vya kampuni hiyo, akisema mbali na hasara kubwa iliyotokea, Watanzania zaidi ya 300 waliokuwa wakifanya kazi kwenye vituo hivyo sasa wako nyumbani bila kazi.
Amesema kampuni hiyo ina wafanyakazi takribani 8,000, huku asilimia kubwa wakiwa Watanzania. Katika vituo takribani 38 vilivyochomwa moto Tanzania nzima, Mtemi amesema vilikuwa na wafanyakazi zaidi ya 300 ambao kwa sasa wamepewa likizo bila malipo.
“Kwa habari tulizozisikia mitandaoni na mitaani, watu wengi wanahusisha Lake Oil na wanasiasa. Inaelezwa kuwa hilo ndilo lilisababisha washambuliaji kufanya vurugu na kuharibu mali kwa lengo la kuwafikia wanasiasa,” amesema.

Amefafanua kuwa kampuni ya Lake Oil ni mali ya Mtanzania mzawa anayeitwa Ally Adha Awadhi, na kwamba hana uhusiano wa aina yoyote na wanasiasa wanaotajwa, wala hawana umiliki wowote ndani ya kampuni hiyo.

Amesema si haki kwa wananchi kuharibu mali ya Lake Oil kwa kudhani inamilikiwa na wanasiasa, kwani hatua hiyo inaathiri maisha ya wafanyakazi pamoja na mmiliki wa kampuni.

Hata hivyo, Mtemi ametoa pole kwa wananchi wote walioathirika kwa namna moja au nyingine na vurugu zilizoibuka kufuatia uchaguzi mkuu wa Oktoba 29.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news