Magazeti leo Novemba 12,2025

HALMASHAURI ya Mji Handeni imeainisha mikakati mitano ya kuimarisha utekelezaji wa afua za lishe, ili kukabiliana na changamoto za utapiamlo na kupunguza idadi ya watoto wanaozaliwa wakiwa na uzito pungufu.
Akisoma taarifa ya Tathmini ya Utekelezaji wa Afua za Lishe kwa Robo ya Kwanza, Novemba 11, 2025, Ofisa Lishe wa Halmashauri hiyo, Ester Herman, amesema mikakati hiyo inalenga kuongeza uelewa wa jamii kuhusu lishe bora na kuhakikisha huduma muhimu za lishe zinatolewa kikamilifu katika ngazi zote.

Ametaja baadhi ya mikakati hiyo kuwa ni kuhamasisha jamii kuhakikisha watoto chini ya miaka mitano wanaendelea kuhudhuria kliniki hata baada ya kukamilisha chanjo, na kushirikiana na idara za Elimu Msingi, Sekondari pamoja na Kamati za Lishe za Kata kuhamasisha wazazi kuchangia huduma za chakula shuleni.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news