Magazeti leo Novemba 14,2025

Jeshi la Polisi Mkoa wa Mbeya linamshikilia Tadesa Limoli (32) raia wa nchini Ethiopia na wenzake 37 wote wanaume kwa kosa la kuingia nchini kinyume cha sheria.
Watuhumiwa walikamatwa mnamo Novemba 11, 2025 huko katika Pori la ranchi ya Matebete lililopo katika Kijiji cha Igumbilo Shamba, Kata ya Chimala, Tarafa ya Ilongo, Wilaya ya Mbarali, Mkoani Mbeya wakisafiri kwa kutumia Gari yenye namba za usajili T.953 DJF aina ya Toyota Noah mali ya Stanslaus Mazengo [51] Mkazi wa Isitu ambaye ndiye alikuwa akiendesha Gari hiyo.

Mtuhumiwa Stanslaus Mazengo ameeleza kuwa alikuwa akiwapeleka kuwahifadhi Wahamiaji hao kwenye nyumba ya Jackline Malya [26] Mkazi wa Chimala. Watuhumiwa walikuwa wakiwasafirisha Wahamiaji hao kwa njia ya kificho kwa lengo la kuwapeleka nchini Afrika ya Kusini.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news