Magazeti leo Novemba 15,2025

MKUU wa Mkoa wa Dodoma Mhe. Rosemary Senyamule,amewatembelea wanafunzi wa shule ya sekondari Mtera Dam katika Wilaya ya Mpwapwa na kuwapa pole kufuatia madhila ya kuunguliwa na Bweni hapo Novemba 12, 2025 na kupoteza kila kitu hali iliyoulazimu uongozi wa Wilaya hiyo kufanya utaratibu wa kuwahamishia kwenye shule mbili za Mazae na Kimaghai ili waweze kuendelea na masomo.
Mhe. Senyamule alifika shule moja wapo ya Mazae Novemba 13, 2025 akiwa ameambatana na Katibu Tawala Mkoa wa Dodoma Dkt. Khatibu Kazungu, Kamati ya Usalama Mkoa na Afisa Elimu Mkoa ambapo wametoa baadhi ya mahitaji muhimu yatakayowawezesha wanafunzi hao wa kike kuweza kuendelea na masomo yao pasi na changamoto yeyote.

Akizungumza na wanafunzi hao, Mhe. Senyamule amesema jambo jema la kumshukuru Mungu ni kwamba hakuna maisha ya mwanafunzi yeyote yaliyopotea zaidi ya vitu tu ambavyo vinaweza kutafuta ila uhai wa mtu hauwezi kutafutwa.












Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news