Magazeti leo Novemba 24,2025

Naibu Waziri, Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), anayeshughulikia masuala ya afya, Dkt. Jafari Rajabu Seif, amewataka watumishi wa afya nchini kuhakikisha wanatumia lugha ya upole na staha wanapowahudumia wagonjwa katika vituo vya afya na zahanati za Serikali.
Dkt. Seif ametoa wito huo wakati wa ziara ya kushtukiza katika Kituo cha Afya cha Nyarugusu, kilichopo Kata ya Nyarugusu, Halmashauri ya Wilaya ya Geita.

Serikali ya Dkt. Samia itaendelea kuboresha huduma za afya, ikiwemo ujenzi na ukarabati wa miundombinu ya vituo vya afya na zahanati. Hata hivyo, pamoja na maboresho hayo, nyinyi watoa huduma mna wajibu wa kumpokea mgonjwa kwa tabasamu na kutumia lugha safi, si lugha chafu,” amesema Dkt. Jafari.

Kwa upande wake, Kaimu Mganga Mfawidhi wa kituo hicho, Fredi Feliasian, amesema wamefurahishwa na ziara ya Naibu Waziri huyo akibainisha kuwa kituo hicho kinahudumia wananchi wengi na kinahitaji maboresho makubwa ili kuendelea kutoa huduma bora kwa jamii.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news