Mheshimiwa Dkt.Mwigulu Nchemba aapa bungeni kutumikia wananchi wa Iramba Magharibi

DODOMA-Mbunge wa Jimbo la Iramba Magharibi kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba, ameapishwa rasmi leo Bungeni jijini Dodoma, kuendelea kuwahudumia wananchi wa jimbo lake kwa awamu nyingine.
Baada ya kuapishwa, Dkt. Nchemba ameahidi kuendeleza juhudi za kuwaletea wananchi maendeleo endelevu, akisisitiza dhamira yake ya kuimarisha miradi ya kijamii na kiuchumi inayolenga kuinua ustawi wa wananchi wa Iramba Magharibi.
Wananchi wa Iramba Magharibi pamoja na Watanzania kutoka maeneo mbalimbali wameendelea kumpongeza kupitia mitandao ya kijamii, wakieleza imani yao kuwa ataendeleza uongozi wenye tija, uwajibikaji na matokeo chanya kwa Taifa.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news