Rais Dkt.Mwinyi ashiriki uzinduzi wa Bunge la 13 la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

DODOMA-Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Mhe. Dkt. Hussein Ali Mwinyi ameshiriki Uzinduzi wa Bunge la 13 la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, uliofanyika leo tarehe 14 Novemba 2025 katika Ukumbi wa Bunge jijini Dodoma.
Bunge hilo la 13 limezinduliwa rasmi na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, mara baada ya kulihutubia kwa kuweka mwelekeo wa Serikali katika kipindi cha pili cha utekelezaji wa Serikali ya Awamu ya Sita.
Hafla hiyo imehudhuriwa na viongozi mbalimbali wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, Viongozi Waastafu SMT na SMZ, Mabalozi wanaoziwakilisha nchi zao Tanzania, Wakuu wa Vyombo vya Ulinzi na Usalama wastaafu na walioko madarakani, Vyama vya Siasa, Viongozi wa Dini na Wageni waalikwa.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

Know matter how large or small your business is, advertising here