Rais Dkt.Samia azindua Tume Huru ya Uchunguzi wa Matukio ya Siku ya Uchaguzi Mkuu,2025

NA DIRAMAKINI

RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan amezindua rasmi Tume Huru ya Uchunguzi ya Matukio ya Uvunjifu wa Amani yaliyotokea wakati na baada ya Uchaguzi Mkuu wa tarehe 29 Oktoba, 2025.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa na Katibu Mkuu Kiongozi Balozi Dkt. Moses Kusiluka, Mwenyekiti wa Tume Huru ya Uchunguzi wa Matukio ya Uvunjifu wa Amani yaliyotokea wakati na baada ya Uchaguzi Mkuu uliofanyika tarehe 29 Oktoba, 2025, Jaji Mkuu Mstaafu wa Mahakama ya Tanzania Mohamed Chande Othman katika picha ya pamoja na Wajumbe wa Tume hiyo, Ikulu Chamwino, tarehe 20 Novemba, 2025.

Halikadhalika, alisema Tume itapatiwa hadidu za rejea ikiwemo uchunguzi wa kina wa chanzo cha matukio hayo, mienendo ya wadau mbalimbali wa siasa na jamii, pamoja na hatua zilizochukuliwa kukabiliana na vurugu hizo na mazingira yaliyohatarisha amani na kusababisha madhara kwa wananchi na Serikali.
Mwenyekiti wa Tume Huru ya Uchunguzi wa Matukio ya Uvunjifu wa Amani yaliyotokea wakati na baada ya Uchaguzi Mkuu uliofanyika tarehe 29 Oktoba, 2025, Jaji Mkuu Mstaafu wa Mahakama ya Tanzania Mhe. Mohamed Chande Othman akiwa pamoja na Wajumbe wa Tume hiyo kabla ya kuzinduliwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, Ikulu Chamwino mkoani Dodoma tarehe 20 Novemba, 2025.
Rais Dkt. Samia aliunda Tume hiyo tarehe 18 Novemba, 2025 kwa mujibu wa Sheria ya Tume za Uchunguzi ya mwaka 2023 (Sura ya 32). Tume itakuwa chini ya uenyekiti wa Jaji Mkuu Mstaafu, Mheshimiwa Mohamed Chande Othman, na imepewa muda wa miezi mitatu ya utekelezaji wa jukumu hilo.

Akizungumza wakati wa uzinduzi, Rais Dkt. Samia amewashukuru wajumbe wa Tume kwa kukubali jukumu hilo muhimu kwa maslahi ya Taifa na kusisitiza kuwa ana imani na uwezo wao wa kulitekeleza jukumu hili kubwa kwa weledi na uadilifu.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan akizungumza na viongozi mbalimbali Ikulu Chamwino mkoani Dodoma tarehe 20 Novemba, 2025 kabla ya kuzindua Tume Huru ya Uchunguzi wa Matukio ya Uvunjifu wa Amani yaliyotokea wakati na baada ya Uchaguzi Mkuu uliofanyika tarehe 29 Oktoba, 2025.
Katika hatua nyingine, alisisitiza kuwa kazi na mapendekezo ya Tume hiyo yataweka msingi kuelekea uundwaji wa Tume ya Mazungumzo na Maridhiano kama alivyoahidi kuiunda katika siku 100 za mwanzo za muhula wa pili wa uongozi wake.
Viongozi mbalimbali waliohudhuria hafla ya uzinduzi wa Tume Huru ya Uchunguzi wa Matukio ya Uvunjifu wa Amani yaliyotokea wakati na baada ya Uchaguzi Mkuu uliofanyika tarehe 29 Oktoba, 2025. Hafla hiyo ilifanyika Ikulu Chamwino mkoani Dodoma tarehe 20 Novemba, 2025.
Rais Dkt. Samia amesema kwamba uamuzi wa kuunda Tume ya ndani umetokana na umuhimu wa Taifa kujitathmini lenyewe na kwamba mapendekezo yake yatatoa dira muhimu ya kusonga mbele kama Taifa linalothamini amani, utulivu na mshikamano.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

Know matter how large or small your business is, advertising here