Rais Dkt.Samia ateua Katibu Mkuu na Naibu Katibu Mkuu wa Ofisi ya Rais,Maendeleo ya Vijana

NA DIRAMAKINI

RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, amefanya uteuzi wa viongozi wawili.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi Dkt. Moses Kusiluka, viongozi walioteuliwa ni wafuatao:-

(i) Bi. Jenifa Christian Omolo, ameteuliwa kuwa Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais,Maendeleo ya Vijana. Kabla ya uteuzi huu, Bi. Omolo alikuwa Naibu Katibu Mkuu, Wizara ya Fedha; na

(ii) Dkt. Kedmon Elisha Mapana, ameteuliwa kuwa Naibu Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, Maendeleo ya Vijana. Kabla ya uteuzi huu, Dkt. Mapana alikuwa Katibu Mtendaji, Baraza la Sanaa la Taifa.

Aidha, uapisho wa viongozi walioteuliwa utafanyika Ikulu Chamwino, Dodoma tarehe 21 Novemba, 2025 saa 8.00 mchana.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

Know matter how large or small your business is, advertising here