TFF yasitisha mkataba wa Kocha Mkuu wa Taifa Stars

DAR-Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) limesitisha kwa makubaliano ya pande mbili mkataba wa Kocha Mkuu wa timu ya Taifa, Taifa Stars, Hemed Suleiman Morocco.
Kutokana na hatua hiyo, TFF imemteua Kocha Miguel Gamondi wa Singida Black Stars kuwa Kaimu Kocha Mkuu wa Taifa Stars. 

Mazungumzo kati ya TFF na Singida Black Stars tayari yamekamilika ili kuhakikisha kocha huyo anachukua majukumu mapya kwa utaratibu mzuri.

Kocha Gamondi ndiye atakayeiongoza Taifa Stars kwenye Fainali za AFCON zitakazofanyika nchini Morocco kuanzia Desemba mwaka huu.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news