Wanafunzi waitwa vyuoni kuanza masomo kote nchini

DODOMA-Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia inapenda kuutarifu umma kuwa, kwa mujibu wa kalenda ya kitaaluma ya mwaka wa masomo 2025/2026, vyuo vyote vya elimu ya kati na ya juu, vya umma na binafsi, vitafunguliwa kama ifuatavyo:

Wanafunzi wa mwaka wa kwanza wanatakiwa kuripoti vyuoni kwa ajili ya programu ya utangulizi (orientation programme) kuanzia Novemba 17, 2025, kabla ya kuanza rasmi kwa masomo.

Wanafunzi wanaoendelea watarudi vyuoni kuanza rasmi masomo kuanzia Novemba 24, 2025.

Wizara inawahimiza wanafunzi wote kuhakikisha wanawasili vyuoni kwa wakati, kufuata ratiba zilizopangwa, na kushiriki kikamilifu katika shughuli zote za kitaaluma.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news