Waziri Dkt.Kijaji,Chande ziarani mkoani Morogoro

MOROGORO-Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Dkt.Ashatu Kijaji, akiwa pamoja na Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Hamad Chande, wamewasili mkoani Morogoro na kupokelewa na Mkuu wa Mkoa wa Morogoro, Mhe. Adam Malima, kwa ajili ya kuanza ziara ya kikazi mkoani humo.
Katika ziara hiyo, Mhe. Dkt. Kijaji na Mhe. Chande wanatarajiwa kutembelea Mamlaka ya Usimamizi wa Wanyamapori Tanzania (TAWA) pamoja na Hifadhi ya Taifa ya Mikumi.
Lengo la ziara hii ni kujifunza, kujionea shughuli mbalimbali za uhifadhi na utalii pamoja na kujitambulisha katika taasisi zilizo chini ya Wizara ya Maliasili na Utalii.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news