DCEA,TAKUKURU watoa elimu dhidi ya dawa za kulevya IAA Kampasi ya Babati

MANYARA-Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya (DCEA) Kanda ya Kaskazini kwa kushirikiana na Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) Mkoa wa Manyara imetoa elimu kinga juu ya madhara ya tatizo la dawa za kulevya kwa wanafunzi wa mwaka wa kwanza katika Chuo cha Uhasibu (IAA) Kampasi ya Babati mkoani Manyara.
Elimu hiyo iliyotolewa katika program ya Orientation ilikazia uhusiano wa Rushwa na Dawa za Kulevya.
Pia, wanafunzi walihamasishwa kutojihusisha na dawa za kulevya ili waweze kutimiza ndoto zao.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news