Abiria wanaosafiri kwa njia ya reli wahakikishiwa usalama wa safari zao

ARUSHA-Kamanda wa Polisi Kikosi cha Reli Tanzania, Kamishna Msaidizi wa Polisi (ACP) Matride Kuyeto amewahakikishia abiria wanaosafiri kwa njia ya reli kuwa,Jeshi la Polisi limejipanga kikamilifu kuhakikisha usalama wao wakati wote wa safari.
Akizunguma leo Desemba 2, 2025 katika Stesheni ya Reli ya jijini Arusha, ACP Kuyeto aliwahakikishia abiria wanaosafiri kutoka Arusha kuelekea Dar es Salaam kuwa njia ya reli ni salama na imeimarishwa kwa ulinzi wa kutosha.
“Niwahakikishie usalama katika safari yenu, na niwahakikishie kuwa mumechagua njia sahihi na salama ya usafiri wa reli kwa kuwa askari wetu wapo imara kabla na wakati wote wa safari mkiwa ndani ya treni,”amesema ACP Kuyeto.

Aidha, Kamanda huyo aliwahimiza abiria kuwa mabalozi wa amani katika jamii zao, akibainisha kuwa amani ni msingi muhimu wa maendeleo ya mtu binafsi na taifa kwa ujumla.
Jeshi la Polisi Kikosi cha Reli limeendelea kuimarisha doria na ulinzi katika maeneo mbalimbali ya reli nchini, likilenga kutoa huduma salama na ya kuaminika kwa wasafiri.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

Know matter how large or small your business is, advertising here