Magazeti leo Desemba 2,2025

WAZIRI wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu), William Lukuvi amesema kuwa katika maadhimisho ya Siku ya Ukimwi Duniani mwaka 2024 yaliyofanyika mkoani Ruvuma, Serikali ilisambaza matokeo ya utafiti wa hali ya VVU na Ukimwi nchini ambayo yanaonesha kuwa takribani watu milioni 1.7 wanaishi na virusi vya Ukimwi.
Akizungumza jijini Dar es Salaam kwenye kilele cha maadhimisho ya kitaifa ya Siku ya Ukimwi Duniani, Lukuvi alisema matokeo hayo pia yanaonesha mafanikio katika upatikanaji wa huduma za VVU na Ukimwi, ikiwamo ongezeko la watu wanaotambua hali zao za maambukizi kutoka asilimia 91 mwaka 2024 hadi asilimia 92 mwaka huu.

Aidha, amesema kiwango cha watu wanaoishi na VVU (WAVIU) wanaotumia dawa za kufubaza virusi (ARV) kimeongezeka kutoka asilimia 98 mwaka 2024 hadi asilimia 98.5 mwaka huu, hatua aliyoielezea kuwa ni ishara ya kuimarika kwa huduma za afya kwa watu wanaoishi na VVU.























Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news