Nassor Idrissa achaguliwa kuwa Mwenyekiti mpya wa Bodi ya Ligi Kuu Tanzania (TPLB)

DAR-Nassor Idrissa (Father) amechaguliwa kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Ligi Kuu Tanzania (TPLB) baada ya kupata kura saba (7) dhidi ya kura sita (6) za mpinzani wake CPA Hosea Lugano kwenye uchaguzi uliofanyika Novemba 29, 2025 katika Hoteli ya Golden Tulip jijini Dar Es Salaam.
Akizungumza na waandishi wa habari, Nassor alisisitiza chini ya utawala wake atahakikisha haki inapatikana kwa kila timu bila kujali ukubwa wa timu, hususani maamuzi yanayotolewa ndani ya dakika 90 za mchezo.
Katika hatua nyingine,Hassan Muhsini Mwenyekiti wa Coastal Union amechaguliwa kuwa Makamu Mwenyekiti wa Bodi ya Ligi Kuu Tanzania ambapo katika nafasi hiyo hakuwa na mpinzani, hivyo kupitishwa kwa kura ya ndio wajumbe wa Mkutano Mkuu wa Bodi ya Ligi Kuu Tanzania (TPLB).

Pia,Japhet Makau Rais wa Fountain Gate na Gilbert Nkolonko Mwenyekiti wa Mbeya City wamechaguliwa kuwa wajumbe wawakilishi wa klabu za Ligi Kuu ya NBC Tanzania Bara.
Aidha, Ahmed Gao wa Bigman na John Ndumbaro wa Mbeya City wamechaguliwa kuwa wajumbe wawakilishi wa klabu za Ligi ya Championship ya NBC wakati huo huo Azim Khan wa Dar City amechaguliwa kuwa mjumbe mwakilishi wa klabu za First League.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news